UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..
26/11/2016.
Baadhi ya wakulima katika kijiji cha Wendele Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga Wameiomba serikali kuwasaidia kuwatafutia mbegu zinazostahimili ukame ili kukabiliana na Baa la njaa.
Kauli hiyo imetolewa na Wakulima hao kufuatia taarifa iliyotangazwa na mamlaka ya hali ya hewa nchini TMA, mapema mwanzoni mwa msimu wa kilimo ambapo mamlaka hiyo ilitoa taarifa kuwa msimu huu wa kilimo kutakuwa na mvua za wastani hivyo wakulima wachukue tahadhari ya kulima mazao yanayostahimili ukame.
Wakulima hao wamesema serikali haina budi kuwaletea mbegu hizo ikiwemo mbegu za mtama, na mihogo ili waweze kuzitumia na kukabiliana na hali itakayokuwepo mwaka huu ya mvua za wastani.
Diwani wa kata hiyo ya wendele Kilunga Justine amesema Wananchi wenyewe wanatakiwa kutambua kuwa suala la kutafuta mbegu zinazostahimili ukame siyo la serikali pekee na kuwahimiza kufanya juhudi zao wenyewe za kupata mbegu hizo.
Zaidi ya kaya 1000 zilizopo katika kijiji cha wendele zina hitaji mbegu hizo zinazostahimili ukame ili kukabiliana na hali ya uwepo wa mvua za wastani iliyotangazwa mwaka huu na mamlaka ya hali ya hewa.
www.ndalike.blogspot.com
LIKE PAGE YETU HAPA CHINI
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA
Post a Comment