0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..


Hatimaye Masomo kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya msingi Mwakata wilayani Kahama, Shinyanga yananza jumatatu baada ya kukatishwa kwa zaidi ya siku 10, kutokana na madasa ya shule hiyo kutumika kuhifadhi  misaada na wananchi waliokuwa wamekubwa na maafa  ya mvua ya mawe yaliyotokea machi 3 mwaka huu katika kata hiyo.


Akizungumza na Nipashe Mwalimu mkuu wa shule hiyo Idd Ginila alisema masomo yameanza rasmi jumatatu ambapo zoezi la awali lilikuwa ni kuwagawia wanafunzi vifaa  vya shule ambavyo ni sehemu ya msaada vilivyotolewa na wananchi, makampuni na taasisi mbalimbali.

Alisema walitumia misikiti, makanisa pamoja na uongozi wa  serikali ya kijiji kuwatangazia wazazi na walezi kuwahimiza wanafunzi, kuhudhuria masomo yao.

“Tulitangaza kuanzia ijumaa kule msikitini, pia tulifanya hivyo siku ya jumamosi na jumapili kutangaza makanisani,  na jumatatu tumegawa vitu vyote vya misaada ambavyo ni madaftari, karamu, penseli na vifaa vingine kwa wanafunzi.”alisema Mwalimu mkuu.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa shule alisema changamoto iliyopo ni ukosefu wa matundu manne ya choo cha wavulana kutokana na kile cha awali kubomolewa na mvua na kwamba kwa sasa wanatumia vyoo vya muda vilivyokuwa vikitumika wakati wa kambi huku uchimbaji wa matundu mengine ukuendelea na utakamilika bada ya siku 14.

Kwa  uapande wake mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya alisema tayari watu waliokuwa katika kambi ya shule ya msingi Mwakata wamekwisha kuhamia katika nyumba zao za muda zilizojengwa na serikali huku baadhi ya watu ambao nyumba zao hazijakamilika wakihamishiwa katika jingo la chuo cha walemavu lililopo kijijini hapo.

Alisaema kufuatia  kukatishwa kwa masomo kwa zaidi ya siku kumi, tayari wameshafanya mpango wa kufidishia siku hizo ambapo wakati wa rikizo fupi wataendelea ka muda wa wiki moja na tayari walimu wamekwishwa kufahamishwa.

LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top