0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..

Na Alfred Bulahya, Kahama.
26/11/2016.

Jamii wilayani Kahama imetakiwa kuhakikisha inatoa ushirikiano kwa vyombo vinavyosimamia suala la ukatili wa kijinsia, kwa kutoa taarifa sahihi na kwa wakati, ili kuwafichua wanaojihusisha na jambo hilo,
Hali  hiyo itasaidia kukomesha  vitendo vya ukatiri  wilayani  humo.

Kauli hiyo imetolewa jana, ijumaa na katibu wa tume ya utumishi wa walimu wilayani Kahama, TSC, Bashemela Seif, kwa niaba ya  mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji wa kahama, Anderson Msumba, katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia nchini.

Seif amesema ni vyema jamii ikashirikiana na vyombo husika ili kukomesha vitendo hivyo ambapo amesema mpaka sasa  matukio   mbalimbali  yanayohusisha  kesi za ukatiLI wa kijinsia na watoto yametolewa taarifa kwa jeshi la Polisi na usatawi wa jamii.

Amesema matukio yanayoongoza tutotewa taarifa serikalini ni  matukio   ya kutelekeza watoto, kutupwa, ajira za utotoni , ukatili wa kimwili,  mimba za utotoni, kubakwa, na kupigwa.
insert bashemela.

Akisoma risala mbele ya mgeni rasimi asikari kutoka Jeshi la Polisi, kitengo cha dawati la jinsia  na watoto, Debora kizanga amesema  licha ya elimu kutolewa kwa wananchi bado wananachi wamekuwa wakishindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi jambo amabalo linasababisha kukosa haki.

Maadhimisho ya siku 16 ya  kupinga ukatiri wa kinjisia hufanyika kila mwaka   kuanzia novemba 25 hadi  disemba 10, na  katika mji wa Kahama maadhimisho  hayo yamezinduliwa katika ukumbi wa bwalo la polisi   huku  kauli mbiu ya mwaka huu ni “funguka pinga ukatili wa kijinsia”.
www.ndalike.blogspot.com

LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top