0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..


Timu ya soka ya Ambasador sc ya mjini Kahama ambayo inashiriki ligi DARAJA LA PILI NGAZI YA Mkoa wa Shinyanga pamoja na Kagongwa United yenye masikani yake katika mji mdogo wa Kagongwa zitacheza mechi ya kirafiki juma pili hii machi 15 mwaka huu.

Mchezo huo ambao utapigwa katika uwanja wa shule ya Msingi Kagongwa ni MAALUM kwa ajili ya kupata fedha ambazo zitawasilishwa kwa waathirika  wa Mvua yam awe iliyoambatana na upepo mkali katika kata ya Mwakata ambapo mchango huo utawasilishwa kupitia kamati ya maafa ya wilaya ya Kahama ambayo imeweka kambi katika kata ya Mwakata.
 

Tayari maandalizi ya mchezo huo yamekamilika ikiwa ni pamoja na  kufanya matangazo katika vijiji vyote vinavyozunguka kata ya kagongwa  pamoja na kupanga utarabu wa viingilio katika mchezo huo ambapo kiingilio kitakuwa ni shilingi 500 kwa kila mshabiki atakayeingia.

Afisa habari wa Klabu ya Ambasador Ndalike Said Sonda “Kocha Mkongwe” aliwataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kyazama mchezo huo  ili kupata fedha nyingi ambazo zitawasilishwa mapema wiki ijao kwa wahusika wa maafa hao.

Aidha alisema, mbali na kiingilio hicho pia wadau wanaruhusiwa kuja na vitu vingine  kama mchele Unga  mabati Mbao kuku n.k ambavyo vitakusanywa tayari kupelekwa  katika kijiji cha Mwakata kwa walengwa.

Sonda alisema  mchezo huo pia utahidhiriwa na viongozi mbalimbali wa chama cha soka wilaya ya Kahama KDFA, Viongozi wa Serikali, Dini na hata Siasa hivyo wananchi wajitokeze kwa wingi kwamni mabli na kuchangia maafa pia timu hizo ni Mahasimu wa kubwa  wa soka hapa wilayani Kahama.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kagongwa United Dogo Mshashi aliiambia blogu hii kwamba  wadau wa soka wanapaswa kukuswa kutokana na mchezo huo ni njia ya kuwakumbuka waathirika  wa maafa hayo pamoja na wale waliopoteza Maisha.

LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top