0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..

Na Amos Lugaila, Kahama.
09/12/2016.
Wananchi wa halmashauri ya Msalala wilayani Kahama wametakiwa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali za kuboresha huduma za afya ili kuongeza ustawi wa jamii  katika halmashauri hiyo.

Hayo yalisemwa leo na Kaimu Mganga mkuu wa halmashauri ya Msalala  Dokta Ignas Lufulila  wakati akizungumza na Baloha fm.

Dokta Lufulila aliwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika kusaidia kupatikana huduma za afya katika jamii.
Alisema, jukumu la kuboresha Huduna za afya kwa jamii siyo la serikali pekee, na hivyo wajitokeze kuchangia ujenzi wa miundombinu ya afya, pamoja na kutunza na kuilinda  miundombinu hiyo.

Aidha Lufulila alitoa wito kwa wananchi  kujiunga katika mfuko wa afya ya jamii CHF kwani mfuko huo ni moja kati ya mikakati ya serikali katika kuboresha huduma za Afya.

www.ndalike.blogspot.com

LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top