0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..




Imeelezwa kuwa nusu ya wanafunzi wanaosoma katika shule ya msingi Mwakata Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga  wameshindwa kuhudhuria masomo yao kutokana na wengi wao kuwa hana sare za shule kutokana na kuharibiwa na mvua ya mawe iliyonyesha machi 3 mwaka huu.



Wanafunzi hao wameshindwa kufika shuleni licha ya jamii kutangaziwa kuwahimiza wanafunzi wahudhuria masomo baada ya kusitishwa kwa muda kutokana na kutokea kwa maafa yaliyosababishwa na mvua ya mawe.

Akizungumza na Nipashe ofisini kwake Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Mwakata, Iddi Ginila alisema shule hiyo ina jumla ya wanafunzi  736  ambapo waliohudhuria masomo kuanzia jumatatu na jumanne ni zaidi ya 340,  huku wanafunzi 53 wakihudhuria masomo bila sare za shule.

Alisema wanafunzi ambao hawajahudhuria masomo sababu kubwa imetajwa kuwa  hawana sare za shule kutokana na makazi yao kusombwa na maji, huku wengine wakiwa familia zao zikihangaikia makazi.

Hata hivyo alisema tayari wamefanya ugawaji wa madaftari kwa wanafunzi waliohudhuria ambapo kila mwanafunzi amepewa Madaftari 9 na zilizobaki zitatolewa kwa wanafunzi ambao bado hawajahudhuria masomo.

Marrynasi Rafael ambaye ni mwalimu wa shule hiyo alipongeza juhudi za serikali kwa kurejesha masomo kwani changamoto kubwa ilikuwa ni kwa wanafunzi wa darasa la nne na darasa la saba ambao wanakabiliwa na mitihani ya taifa.

Nao baadhi ya wanafunzi waliozungumza na Nipashe wamefurahia kuanza kwa masomo huku wakiwataka wanafunzi  wenzao kufika shuleni kuendelea na masomo.

LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top