0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..

Na Faustine Gimu, Kahama
Kundi la watu  wasiao fahamika wamechoma nyumba ya mwenyekiti wa serikali ya Kijiji cha  Mwalugulu kata ya mwalugulu wilayani hapa na kisha kumwandikia barua ya kumtishia maisha yake  wakimtaka ahame katka kijiji hicho.
MOTO MKUBWA WATEKETEZA VIBANDA VILIVYOPO NYUMA YA STENDI YA DALA DALA ...
Tukiko la kuchomwa kwa nyumba hiyo limetokea mwisho mwishon mwa wiki iliyopita  na siku ya juma tatu alikuta  barua hiyo ikimtaka  ahame katika kijiji hicho.

Akizungumza juzi  mwenyekiti huyo alisema  barua hiyo  Paul  Masule aliikuta jirani na zizi lake ikiwa imebandikwa huku ikimtaka ahame aende mbali zaidi kwa usalama wake.

"Nyumba yangu ilichomwa ijumaa iliyopita, halafu jumatatu nilipoamuka nikamwanbiwa mtoto wangu aende kugagua mifugo alipofika aliona  barua ndio akamwita  ili aisome nilipoenda nikaisoma inasema kwamba nihame utemi tisa au  majimbo tisa."alisema Mwenyekiti huyo.

Aidha alisema huenda chazo cha tukio hilo ni kutokana na oporasheni inayoendeshwa katika kijiji hicho cha kuwabaini kwa kuwapigia kura za siri wahalifu.
Naye Kaimu afisa Mtendaji wa Kijiji hicho, Masanja Mathias alisikitishwa na vitisho hivyo ambavyo viongozi wameanza kufanyiwa na aliwaomba wananchi kuwa na Ushirikiano kuwabaini wahalifu..

www.ndalike.blogspot.com

LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top