0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..



WAKAZI wa Kijiji cha Mwakata Wilayani Kahama Mkoani Shinaynga walioathirika na mvua ya mawe iliyonyesha hivi karibuni huwenda wakapata makazi yakudumu na kuhama katika Shule ya msingiMwakata walipokuwa wameweka kambi  kutokana na baadhi ya makampuni ya ujenzi kuanza kutoa misaada kwa ajili ya ujenzi wa makazi mapya.
Baadhi ya Makampuni yalioanza kutoamsaada huo kwa wahanga haonipamoja na Kampuni ya Mwanza huduma Limited Iliyotoa Jumla yamifuko 560 kwa ajili ya kusadia ujenzi wa Makazi mapya kwa wahanga hao pamoja Kampuni ya Airtel Tanzania iliyotoa Jumla ya mabati100.
 
Pia Kampuni Simba Cement ya Jijini Tanga pia imetoa Msaada wa Mchele kilo 1,500, Unga Mahindi kilo 1,500,Mafuta ya kupikia Lita 500  Sukari kilo200,Madaftari Katoni 60, Blankets pisi 300 pamoja na box nne za Kalamu kwa ajili ya Wanafunzi waliokumbwa na matatizo hayo ya Mvua ya mawe.
 
 Kampuni hiyo ya Simba sementi kupitia wakala wake aliyopo Mjini Kahama Engan Enterprises ya Mjini Kahama imehaidi kuendelea kusadia wahanga hasa katika sekta yaujenzi ili waweze kufanikiwa kupata makazi mapyanakuanza kuishi kama ilivyokuwa hapo awali.
 
Kwa upande wake Meneja Biashara wa Kampuni ya Simba Cement Matheus Roose alisema  kuwa misaada hiyo waliotoa wanaimani kuwa itawasaidia wahanga na kuongeza kuwa waokama wadau wameguswa na tukio hilo ambaloni la kihistoria hapa nchini.
 
Kwa uapnde wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga akipokea misaada hiyo alisemakuwa kwa sasa misaada kamahiyo kwa ajili ya Ujenzi ndiyo inahitajika kwa wahanga hao ilikurahisisha kupungua katika kambi nakusababisha Wanafunzi kukosa masomo hadi kufikia hivi sasa.
 
"Wanafunzi hawa wa shule ya Msingi Mwakata waliopo likizo kwa sasa kupisha wahanga hawa lazima waanze shule mara moja na kwa wasamaria wema kuanza kuleta vifaa vya ujenzi kamavile mabati Saruji na vinginevyo vitasadia kwa wahanga hawa kuanza kujenganyumba zao upya na kupunguza msongamano katikashule hiyo”, Alisema Rufunga. 
Pia aliongeza kuwa kwa sasa ni lazima kuhakikisha kuwa wanafunzi wanaanza masoma mara moja na tutaanza mikakati yakuihamisha kambi hii ndani ya sikumbili nikibali tulichopewa naWizara ni cha kuwahifadhi kwa siku hizo na si vinginevyo.

LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top