0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..

Mbunge wa jimbo la Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga Ezekiel Maige ametoa mashine ya kudurufu karatasi kwa shule ya sekondari Mwalimu Nyerere iliyopo Kata ya Segese ili kusaidia uchapishaji wa mitihani wa wanafunzi kufanyika shuleni hapo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mashine hiyo mbele ya  viongozi wa Kata hiyo, wazazi, walimu,na wanafunzi Maige alisema  mashine hiyo ni ahadi aliyoahidi wakati wa mahafari ya kidato cha nne  mwaka jana shuleni hapo huku gharama ya kifaa hicho kikiwa ni shilingi milioni 5.

Alisema  aliamua kuahidi na kutoa msaada huo kutokana na kuwepo kwa changamoto kubwa ya uchapishaji wa mitihani kwa licha ya kwamba shule hiyo ina umeme unaotumia nishati ya Juan a kwamba walimu na wanafunzi waitunze mashine hiyo ili iweze kudumu na kuwasaidia katika kuarahisisha kazi zao.

Katika hatua nyingine Maige aliwapongeza wazazi na walezi wa wanafunzi wa shule hiyo kwa jitihada wanazozionesha katika kuboresha miundombinu ya shule hiyo hali ambayo imesabaisha kuendelea kuinua kiwango cha elimu katika shule hiyo ambapo katika miaka ya hivi karibuni  ni miongoni mwa shule zinazofanya vizuri kwa upande wa taalum mkoani Shinyanga.

Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo  Peter Kweba alisema mashine hiyo itasaidia kupunguza makali ya matumizi ya fedha  kwa shule hiyo  kwani awali walikuwa wakitumia zaidi ya shilingi milioni 12 kwa mwaka ambapo kila mtihani walikuwa wakitumia zadi ya shilingi milioni 3 kudurufu mitihani.

Aidha baadhi ya wazazi na wanafunzi walimpongeza Mbunge Maige kwa kuzidi kujali wananchi wa  jimbo la Msalala katika sekta zote ambapo wakizungumzia msaada huo walisema  imepunguza usumbufu wa michango iliyokuwa ikitolewa kwa ajili ya uchapishaji wa mitihani.



LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top