0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..

Kukamilika kwa mradi wa umeme vijijini katika Kata ya Bulige halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga kutasaidia kuongeza mapato ya ndani yanayokuswanwa na halmashauri hiyo kutokana na kwamba wamekusudia kuweka soko la kimataifa la mchele katika kata hiyo.



Akizungumza na wanachi wa Kijiji cha Segese kata ya Segese, Mbunge wa jimbo la Msalala Ezekiel Maige alisema tayari katika kijiji cha Bulige wametenga eneo kwa ajili ya soko hilo ambalo litasaidia mpunga unaozalishwa katika halmashauri hiyo kukobolewa na kuuzwa katika soko hilo na hivyo kuiingizia  mapato ya ndani halmashauri hiyo.

Maige alisema hali hiyo itasaidia kukusaya ushuri unaotokana na mapato hayo zaidi ya shilingi Milioni 500, kila mwaka hali ambayo itasaidia kuinua uchumi wa wananchi wa halmashauri hiyo.

Alisema mbali na soko hilo pia amebainisha mapato mengine ya ndani ambayo yataisaidia halmashauri kujiendesha ni pamoja na  kupata ushuru  kutoka katika kampuni ya uchimbaji madini ya ACACIA kupitia mgodi wa Bulyanhulu pamoja na makampuni yanayofanya kazi ndani ya mgodi huo ambayo nayo waliingia mkataba wa kulipa ushuru kwa halmashauri.

Maige alisema hali hiyo itasaidia pia  kuwepo kwa mkakati wa kufuta michango mbalimbali kwa wananchi kwani halmashauri itakuwa ikijiendesha yenyewe  bila kutegemea michango ya wananchi.

LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top