0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..

Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA kimetoa msaada wa Mabati 850 sawa na bando 50 ambayo ni ahadi iliyotolea na mwenmyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe kusaidia waathirika wa mvua yam awe katika kata ya Mwakata wilayani Kahama.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Katibu wa chadema, Dr. Wilbroard Slaa alisema msaada huo unathamani wa shilingi Milioni 12, ambapo shilingi milioni 10 ilitolewa na chama hicho kupitia ruzuku inayotolea na serikali kwa chama hicho huku shilingi milioni mbili ilipatikana katika mikutano iliyofanywa na chama hicho mjini Kahama.

Alisema waliambua kununua mabati hayo kutokana na kamati ya mkoa inayoratibu mafa hayo ikiongozwa an mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ali Rufunga kupendekeza vinunuliwa vifaa vya ujenzi  kutokana na kwamba chakula kimekuwa kikitolewa na wadau wengi.

Dr. Slaa aliwataka viongozi kuhakikisha wanasimamia vema ujenzi wa nyumba za kuduma za makazi ya wananchi wa kata ya  Mwakata kama ilivyopendekezwa na rais Jakaya Kikwete alipotembelea eneo hilo kwani  mara nyingi serikali imekuwa ikishindwa kutekeleza kwa wakati majanga ya aina hiyo.

“Niombe tu viongozi wa Shinyanga simamieni waathirika hawa wajengewe nyumba kwa muda mwafaka, unajua Watanzania wengi tanawakatisha tama kutokana na kushindwa kutimiza ahadi zinazotolewa, kule Klosa hadi leo bado watu wananishi kwenye mahema, tangu mimi nikiwa mwenyekiti wa Kamati ya kudumu katika Bunge, Naomba sana Shinyanga Muwe Mfano.”alisema Slaa.

Katika hatua nyingine misaada imeendelea kutolewa  kwa waathirika ambapo kampuni ya simu za Nchini, TTCL lilitoa msaada wa chakula na vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi Milioni 3.

Akizungumza Meneja wa TTCL mkoa wa Shinyanga Peter Kuguru alisema  TTCL imeungana na Watanzania wengeine walioguswa na Maafa hayo huku akiyataka mashirika na watu mbalimbali kuendelea kujitokeza kuwasaidia wananchi  walioathirika.
 

Akipokea Misaada hiyo Mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya alisema misaada hiyo itawafikia walengwa.

picha zote na malunde blogu
www.ndalike.blogspot.com 

LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top