0

UNAWEZA KUJIUNGA NASI HAPA MOJA KWA MOJA ..Bofya HAPA ULIKE PAGE YETU!..



Na Ndalike Sonda, Kahama.
12/11/2016.

Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu amewaagiza   maafisa afya  na mazingira katika Kila kata wilayani humo kuhakikisha wanawafikisha mahakamani wananchi wote wanaokamatwa kwa kosa la kukaidi agizo la usafi wa mazingira katika maeneo yao.

Akizungumza na Waandishi wa habari, Nkurlu amewataka maafisa hao watumie sheria  ya afya ya jamii  namba 1 ya mwaka 2009.

Nkurlu amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi  kesho ili kufanya  usafi katika maeneo yao kama  agizo la serikali ya wilaya hiyo  linavyoelekeza.

Wakati huo huo Nkurlu amewaonya wamiliki wa Migahawa, nyumba za kulala wageni na makampuni ambao wanatiririsha maji machafu kwamba serikali imekusudia kuwachukulia hatua za kisehria.

 

LIKE PAGE YETU HAPA CHINI

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by NDALIKE SONDA MEDIA

Post a Comment

 
Top